KARIBU

KARIBU
Tunakusalimu katika Jina la BWANA wetu YESU KRISTO. karibu katika ukurasa huu maalumu wa USCF CCT UDOM CHAPLAINCY-KITIVO CHA TIBA. USCF ni kifupisho cha maneno machache; UNIVERSITY STUDENTS CHRISTIAN FELLOWSHIP na CCT ni kifupisho cha CHRISTIAN COUNCIL OF TANZANIA. Sisi ni ushirika wa vijana wa vyuo vikuu kutoka makanisa wanachama wa baraza la kikristo Tanzania (CCT). tumekuwa na ukurasa huu maalumu kwa ajili ya Kuhubiri Injili, Kufundisha Neno la Mungu, kupashana habari pamoja na kushauriana. Ni kiu yetu kuwa walioko makazini, majumbani, mashuleni na maeneo mbalimbali waweze kufikiwa na mahubiri/mafundisho yetu yanayotolewa na watumishi mbalimbali waliopo katikati yetu na wale wa nje ya USCF pamoja na wahubiri wa kimataifa. KARIBU TUJIFUNZE NA KUHABARIKA NA MUNGUAKUBARIKI

CHUO KIKUU CHA DODOMA

UMOJA WA WANAFUNZI WA KIKRISTO TANZANIA USCF-TIBA.

Bwana Yesu asifiwe,

Kama tulivotangaziwa kuwa kuanzia tarehe 2 February hadi tarehe 5.february siku ya   jumapili tunatarajia kuwa na zoezi la uchaguzi wa viongozi wapya ndani ya USCF-TIBA. Zoezi la uchaguzi litahusisha chaguzi ndogo ndogo za vikundi mbalimbali ndani ya USCF ambazo zitafanyika tarehe 2 siku ya alhamisi kwa upande wa PRAYS AND WORSHIP na kisha tarehe 4 siku ya jumamosi ni upande wa USCF KWAYA. Uchaguzi mkuu utafanyika tarehe 5 jumapili, ambapo uchaguzi wa jumapili utahusisha ngazi zifuatazo:

KAMATI KUU.

  • Mwenyekiti
  • Makamu mwenyekiti
  • Katibu
  • Katibu msaidizi
  • Mtunza hazina.

KAMATI YA MAOMBI.

  • Mwenyekiti
  • Katibu

KAMATI YA UINJILISTI.

  • Mwenyekiti
  • Katibu

WAZEE WA KANISA

  • Kila block 1,2,.F,G,D,A na BCE.







SIFA ZA MTU ANAYESTAHILI KUCHAGULIWA KATIKA NAFASI YA UONGOZI USCF.

  1. Awe mshiriki kamili wa makanisa yanayounda jumuiya ya umoja wa kikristo Tanzania (CCT).  Kama vile

  • Lutheran.
  • Moravian.
  • Anglican.
  • Merronite.
  • Baptist.
  • Bible church Tanzania.
  • Evangelist church of mbalizi.     Na mengineyo.                                                                                                        

  1. Asiwe finalist (Bsc.N4,Bsc.MW,DN3,PH3 MED LAB3) na pia asiwe MD3
  2. Asiwe mtu aliyewahi kukiuka taratibu,kanuni na maadili ya kikanisa kama vile.

  • Kupata ujauzito nje ya ndoa
  • Koa/kuolewa kinyume na taratibu za kanisa.

  1. Asiwe mtu aliyetengwa na kanisa kutokana na makosa ya kinidhamu.
  2. Awe na sifa za kushiriki meza ya bwana kutokana na taratibu za kanisa lake.
  3. Awe ni mtu ambaye una utayari wa kuwa kiongozi ndani ya USCF.

SIFA ZA MTU ANAYESTAHILI KUMCHAGUA KIONGOZI KATIKA UCHAGUZI

  1. Awe mwana USCF
  2. Awe mtu ambaye anashirikiana na USCF katika vipindi vya ibada hata kama sio mwana USCF.




No comments:

Post a Comment

Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa mwanawe pekee ili kila amwaminiye asipotee bali awe na uzima wa milele. Yohana 3;16