KARIBU

KARIBU
Tunakusalimu katika Jina la BWANA wetu YESU KRISTO. karibu katika ukurasa huu maalumu wa USCF CCT UDOM CHAPLAINCY-KITIVO CHA TIBA. USCF ni kifupisho cha maneno machache; UNIVERSITY STUDENTS CHRISTIAN FELLOWSHIP na CCT ni kifupisho cha CHRISTIAN COUNCIL OF TANZANIA. Sisi ni ushirika wa vijana wa vyuo vikuu kutoka makanisa wanachama wa baraza la kikristo Tanzania (CCT). tumekuwa na ukurasa huu maalumu kwa ajili ya Kuhubiri Injili, Kufundisha Neno la Mungu, kupashana habari pamoja na kushauriana. Ni kiu yetu kuwa walioko makazini, majumbani, mashuleni na maeneo mbalimbali waweze kufikiwa na mahubiri/mafundisho yetu yanayotolewa na watumishi mbalimbali waliopo katikati yetu na wale wa nje ya USCF pamoja na wahubiri wa kimataifa. KARIBU TUJIFUNZE NA KUHABARIKA NA MUNGUAKUBARIKI

MATANGAZO


Tunawataarifu kuwa Jumapili ya wiki hii itakuwa mwisho wa kukusanya mchango wa sendoff

No comments:

Post a Comment

Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu hata akamtoa mwanawe pekee ili kila amwaminiye asipotee bali awe na uzima wa milele. Yohana 3;16